• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba District Council
Bukoba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zitolewazo
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Ugani Kilimo
    • Huduma Ugani za Mifugo na Uvuvi
    • Mikopo ya Vikundi vya Wanawake na Vijana
  • Madiwani
    • Madiwani wa Sasa Waliochaguliwa
    • Kamati za Halmashauri
    • Mitasari ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Mfuko wa Taifa wa Maendeleo wa Jamii (TASAF)
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Sheria
    • Ripoti
    • Fomu Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Maktaba ya Picha

Mifugo na Uvuvi



MAJUKUMU YA IDARA YA MIFUGO NA UVUVI

 

 

Mkuu Wa Idara Ya Idara Ya Mifugo Na Uvuvi

Jina: Dr. Kisanga Wiliam Makigo

Simu: +255(0) 685107371

Barua Pepe: kisanga.makigo@bukobadc.go.tz

 

A: Utangulizi:

 Uongozi wa Idara ya Mifugo na Uvuvi ni kama ifuatayo:-



B: Muundo wa Idara:

 

C: Huduma zitolewazo na Idara:

Sekta ya Mifugo: 

Ili kuendeleza ufugaji bora na wa kisasa, Idara inatekeleza majukumu yafuatayo;

Kutoa huduma za ugani wa mifugo kwa wafugaji

Kutoa kinga na tiba kwa mifugo dhidi ya magonjwa mbalimbali

Kuhamasisha na kusimamia uogeshaji wa mifugo katika majosho

Kuhamasisha na kusimamia uboreshaji wa mifugo kwa njia ya uhamilishaji na madume bora ili kupata mifugo bora

Kuhakikisha upatikanaji wa miundombinu ya mifugo ikiwemo malambo, vibanio na majosho

Kusimamia uchinjaji wa mifugo katika machinjio ili kupata nyama inayostahili kwa matumizi ya binadamu.

  • Kukusanya maduhuri ya Serikali kulingana na sheria

Kuhamasisha wananchi na wawekezaji kuwekeza viwanda katika Sekta ya mifugo

  • Sekta ya Uvuvi:
  • Huduma zitolewazo na sekta ya Uvuvi katika kusimamia uvuvi katika ziwa na kutoa elimu ya ufugaji wa samaki ni kama ifuatavyo;
  • Kutoa huduma za ugani kwa wavuvi na wananchi wanaohitaji
  • Kuhakikisha matumizi ya zana za uvuvi endelevu katika ziwa
  • Kutoa elimu juu ya ufugaji endelevu wa samaki kwenye vizimba na mabwawa
  • Kukusanya maduhuri ya Serikali kulingana na sheria
  • Kuandaa na kuhuisha kulingana na wakati rejesta ya wavuvi na wafugaji wa samaki

D. Vituo vilivyoko kwenye Idara: Ili kuhamasisha ufugaji bora vijijini, vituo vya wakulima na wafugaji vifuatavyo hutoa hudua za mafunzo na ugani kwa wafugaji;

Mushozi

Kyema

Nyakibimbili

Kabirizi

Kikomelo

Kyamulaile.

 

E. Mpango wa Idara: 

Kwa mwaka wa fedha 2017/2018 Idara itatekeleza miradi ya maendeleo kama ilivyoandaliwa kwa kushirikiana na wananchi katika maeneo ya Vijiji na Kata kwa kutumia mbinu shirikishi jamii ya fursa na vikwazo kwa maendeleo (O & OD) . Aidha, Sera na miongozo ya Kitaifa inayosimamia sekta ya Mifugo ikiwemo Mkakati wa Kuendeleza Sekta ya Mifugo (Livestock Sector Development Strategy) na Sera ya Mifugo ya mwaka 2007 pamoja na Sera ya Uvuvi ya mwaka 2015 vimezingatiwa kikamilifu.  Mpango wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri wa mwaka 2017/18 una malengo yafuatayo;

Kupunguza vifo vya Mifugo kutoka 7% hadi 5% ifikapo Juni 2020

Kuongeza uzalishaji wa samaki kwa kuongeza mabwawa ya kufugia samaki kutoka 57 hadi 80 ifikapo Juni 2020

Kuwa na mialo iliyoboreshwa kutoka 7 hadi 10 ifikapo Juni 2020

Kuongezeka kwa wafugaji na wavuvi wanaopata huduma za ugani kutoka 4112 hadi 6875 ifikapo Juni 2020

Mpango huu utatekelezwa kwa kutumia vyanzo vya fedha vifuatavyo:

Ruzuku ya Maendeleo ya Serikali za Mitaa (LGCDG)             =          45,000,000

Mapato ya Ndani                                                                        =          18,000,000

Ruzuku ya matumizi mengineyo                                              =          14,258,589

Shughuli zilizolengwa kutekelezwa ni

Kuwezesha kutengeneza mabwawa ya kufugia samaki 25 katika vijiji vya  Rushaka, Butainamwa, Kasharu, Butulage, Mugajwale, Migara, Buzi na Kyema ifikapo Juni 2017 = sh 45,000,000

Kujenga uzio katika mnada wa mifugo katika Kijiji cha Nsheshe = sh 18,000,000

Kutoa huduma za ugani kwa wafugaji na wavuvi = sh 14,258,589

 

F. Mafanikio: Idara ya mifugo na uvuvi katika kutekeleza majukumu yake imepata mafanikio yafuatayo:-

Idadi ya wafugaji na wavuvi wanaopata huduma za ugani imeongezeka kutoka 3,625 hadi 4,900

Kiasi cha maziwa yanayozalishwa kwa mwaka yameongezeka

Magonjwa yaenezwayo na kupu yamepungua kutoka 7% hadi 6%

Mapato yatokanayo na uvuvi yameongezeka.

Idadi ya wafugaji samaki wanaopata huduma za ugani imeongezeka na mabwawa ya samaki yameongezeka  kutoka 57 hadi 69

 

G. Changamoto: Zipo changamoto zinazoathiri utoaji wa huduma za ugani kama ifuatavyo:-

Wafugaji kutokuwa tayari kuchangia gharama za matibabu na chanjo.

Ufinyu wa bajeti kwa uendeshaji wa sughuli za utoaji wa huduma na kugharimia miradi ya maendeleo

Serikali za vijiji kutotenga maeneo ya wakulima na wafugaji

Uhaba wa vitendea kazi

Uhaba wa wataalam

Uvuvi wa kutumia zana haramu zisizoruhusiwa kwa mujibu wa sheria

 


Matangazo Madogo Madogo

  • UMITASHUMTA July 20, 2022
  • UJUMBE WA SENSA TOKA KWA MKURUGENZI MTENDAJI BDC July 23, 2022
  • MWENYEKITI NA SENSA July 23, 2022
  • MRADI WA WODI ZA UPASUAJI July 23, 2022
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • BUKOBA DC YAZINDUA CHANJO YA KUKU

    July 01, 2025
  • MAPATO JUU,HATI SAFI MEZANI

    June 16, 2025
  • MITI MIA TANO YAPANDWA MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI

    June 05, 2025
  • WALENGWA TASAF WATEKELEZA MIRADI YA AJIRA ZA MUDA MFUPI

    May 29, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fomu mbali mbali
  • Picha mbali mbali
  • We are Implementing 2017 (Picha)

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  • Tovuti ya Wizara ya Afya
  • Tovuti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania

Waperuzi Walipo

world map hits counter

Kihesabu Waperuzi

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Bujunangoma

    Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera

    Simu ya Mezani: 028-2220287

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.