• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba District Council
Bukoba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zitolewazo
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Ugani Kilimo
    • Huduma Ugani za Mifugo na Uvuvi
    • Mikopo ya Vikundi vya Wanawake na Vijana
  • Madiwani
    • Madiwani wa Sasa Waliochaguliwa
    • Kamati za Halmashauri
    • Mitasari ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Mfuko wa Taifa wa Maendeleo wa Jamii (TASAF)
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Sheria
    • Ripoti
    • Fomu Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Maktaba ya Picha

DC SIMA AZINDUA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU YA NG'OMBE

Tarehe ya Kuwekwa: September 4th, 2025

Na.Abel Shema

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mhe. Erasto Sima amezindua zoezi la chanjo ya homa ya ng'ombe pamoja na utambuzi wa mifugo kwa kutumia hereni za kieletroniki.

Zoezi hilo limefanyika katika josho la Ntoma,kata ya Kanyangereko Septemba 03,2025.

Akizungumza katika uzinduzi huo DC  Sima alisema Serikali ya Mhe.Dkt.Samia Suluhu Hassan imeleta chanjo hii kwa ruzuku asilimia 50 kwani gharama halisi ya chanjo ni sh 1000 lakini Serikali imechangia nusu ya gharama hivyo mfugaji atalipia sh 500 pekee.

Mhe. Sima alieleza katika Halmashauri ya  Wilaya  Bukoba jumla ya Ng'ombe 37,000 zitapatiwa chanjo pamoja na kuwekewa hereni maalum za kielektroniki kwaajili ya utambuzi wa mifugo hiyo.


Nae mratibu wa chanjo ya mifugo kutoka Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Laurent Buchakundi alieleza kuwa ugonjwa wa CBPP (Contagious Pleuropneumonia) ni homa kali ya mapafu ya ng'ombe inayosababishwa na bacteria waitwao mycoplasma mycoides ambao huenea kwa njia ya hewa kutoka kwa ng'ombe mmoja hadi mwingine

Buchakundi aliongeza kuwa  chanjo hii itasaidia wafugaji kutunza kipato chao kwa kuwa na ng'ombe waliokingwa na magonjwa lakini  pia utambuzi wa mifugo utasaidia usalama na ufuatiliaji wa karibu pale inapohitajika.


Akihitimisha zoezi hili DC Sima aliwakumbusha Wananchi kushiriki Uchaguzi Mkuu Oktoba chini ya kauli mbiu isemayo "Jitokeze Kushiriki Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 kwa Amani na Utulivu".


Viongozi wengine waliohudhuria katika hafla hiyo ni Katibu Tawala Wilaya ya Bukoba Bi.Proscovia Jaka Mwambi na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Bi. Fatina Hussein Laay.

Matangazo Madogo Madogo

  • UMITASHUMTA July 20, 2022
  • UJUMBE WA SENSA TOKA KWA MKURUGENZI MTENDAJI BDC July 23, 2022
  • MWENYEKITI NA SENSA July 23, 2022
  • MRADI WA WODI ZA UPASUAJI July 23, 2022
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • DC SIMA AZINDUA CHANJO YA HOMA YA MAPAFU YA NG'OMBE

    September 04, 2025
  • KARIBU MWENGE WA UHURU KITAIFA MWAKA 2025

    September 02, 2025
  • BUKOBA DC YAZINDUA VAZI LA IJUMAA

    August 15, 2025
  • BUKOBA DC YAZINDUA VAZI LA IJUMAA

    August 15, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fomu mbali mbali
  • Picha mbali mbali
  • We are Implementing 2017 (Picha)

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  • Tovuti ya Wizara ya Afya
  • Tovuti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania

Waperuzi Walipo

world map hits counter

Kihesabu Waperuzi

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Bujunangoma

    Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera

    Simu ya Mezani: 028-2220287

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.