• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba District Council
Bukoba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zitolewazo
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Ugani Kilimo
    • Huduma Ugani za Mifugo na Uvuvi
    • Mikopo ya Vikundi vya Wanawake na Vijana
  • Madiwani
    • Madiwani wa Sasa Waliochaguliwa
    • Kamati za Halmashauri
    • Mitasari ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Mfuko wa Taifa wa Maendeleo wa Jamii (TASAF)
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Sheria
    • Ripoti
    • Fomu Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Maktaba ya Picha

DC SIMA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA BIASHARA WILAYA YA BUKOBA

Tarehe ya Kuwekwa: November 28th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba, Mhe. Erasto Sima, ameongoza kikao cha Baraza la Biashara la Wilaya ya Bukoba kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba, ambapo masuala muhimu ya kuboresha mazingira ya biashara na kuhamasisha uwekezaji yamejadiliwa kwa kina.


Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Mkuu wa Wilaya Mhe. Erasto Sima, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza hilo, alisisitiza umuhimu wa wadau kushirikiana kuboresha mazingira ya biashara ikiwa ni pamoja na kuimarisha usalama,usafi wa mazingira na kuangalia uwezekano wa kufanya biashara masaa 24. Alisema:

“Wilaya ya Bukoba ina fursa nyingi za kiuchumi ambazo zikitumika ipasavyo zitachochea uwekezaji na kuongeza ajira. Serikali iko tayari kushirikiana na sekta binafsi ili kuhakikisha tunafungua milango zaidi ya maendeleo.”

Kwa upande wake, Mbunge Mhe. Mutasingwa alisisitiza haja ya kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wafanyabiashara kwa ajili ya ustawi wa uchumi wa Wilaya huku akiahidi kusimamia mikopo ya wafanyabiashara wadogo kwa kushirikiana na vyama vyao na benki ya NMB.


Akinukuliwa alisema:

“Baraza hili ni jukwaa muhimu kwa sababu linatupa nafasi ya kusikiliza changamoto zenu na kuona namna ya kuziwekea majibu ya haraka. Lengo letu ni kuhakikisha Bukoba inakuwa kitovu cha biashara na fursa kwa wawekezaji.”


Wadau wa biashara nao hawakusita kutoa maoni yao kuhusu namna ya kuimarisha mazingira ya biashara na kuongeza tija kwenye miradi mikubwa ya kimkakati.


Mwakilishi kutoka SHIUMA Bukoba, Bi. Husna Mohamed Abdallah, ambaye ni Katibu wa SHIUMA Mkoa wa Kagera, alisema:

“Tunapongeza juhudi za Serikali kutusikiliza. Changamoto nyingi za wafanyabiashara zinaweza kutatuliwa kwa mawasiliano ya moja kwa moja kama haya. Tunaona mwanga mpya wa ushirikiano.”


Naye mwakilishi wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania – Bukoba (JWT), Bw. Nicholaus J. Basimaki, ambaye ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania Mkoa wa Kagera, alisisitiza umuhimu wa kupunguza urasimu ili kuvutia zaidi wawekezaji. Alisema:

“Urahisishaji wa taratibu za vibali na leseni ni jambo muhimu. Tukipunguza urasimu, hakika idadi ya wawekezaji itaongezeka na pato la wilaya litakuwa kubwa zaidi.”

Kikao hicho kiliangazia pia fursa za uwekezaji katika miradi mikubwa, ikiwemo sekta ya kilimo, utalii, viwanda vidogo na biashara za kimkakati zinazolenga kuinua uchumi wa Wilaya ya Bukoba.


Kikao hicho kimehudhuriwa na Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini, Mhe. Johnston J. Mutasingwa; Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya ya Bukoba; pamoja na wadau mbalimbali wa biashara kutoka taasisi na jumuiya tofauti zikiwemo TCCIA, Jumuiya ya Wafanyabiashara Tanzania – Bukoba, na SHIUMA Bukoba.

Matangazo Madogo Madogo

  • UMITASHUMTA July 20, 2022
  • UJUMBE WA SENSA TOKA KWA MKURUGENZI MTENDAJI BDC July 23, 2022
  • MWENYEKITI NA SENSA July 23, 2022
  • MRADI WA WODI ZA UPASUAJI July 23, 2022
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • DC SIMA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA BIASHARA WILAYA YA BUKOBA

    November 28, 2025
  • PONGEZI

    November 04, 2025
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI

    October 03, 2025
  • BUKOBA DC KUUZA VIWANJA VILIVYOPIMWA

    September 25, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fomu mbali mbali
  • Picha mbali mbali
  • We are Implementing 2017 (Picha)

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  • Tovuti ya Wizara ya Afya
  • Tovuti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania

Waperuzi Walipo

world map hits counter

Kihesabu Waperuzi

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Bujunangoma

    Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera

    Simu ya Mezani: 028-2220287

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.