• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba District Council
Bukoba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zitolewazo
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Ugani Kilimo
    • Huduma Ugani za Mifugo na Uvuvi
    • Mikopo ya Vikundi vya Wanawake na Vijana
  • Madiwani
    • Madiwani wa Sasa Waliochaguliwa
    • Kamati za Halmashauri
    • Mitasari ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Mfuko wa Taifa wa Maendeleo wa Jamii (TASAF)
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Sheria
    • Ripoti
    • Fomu Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Maktaba ya Picha

KAGERA KUJA NA MPANGO MKAKATI KUPUNGUZA UDUMAVU

Tarehe ya Kuwekwa: August 15th, 2025



Na.Abel Shema,Bukoba


Hayo yamesemwa katika kikao maalum cha kuwasilisha mipango mikakati ya kupunguza udumavu kutoka katika Halmashauri zote 8 za Mkoa wa Kagera, kilichofanyika Agosti 14,2025 katika ukumbi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera.


Akizungumza katika kikao hicho kaimu katibu tawala mkoa wa Kagera Ndugu,Bwai Biseko alieleza mpango huu ni wa miaka 3 ukiwa na  lengo la  kupunguza tatizo la udumavu katika mkoa wa Kagera kutoka asilimia 34.3 mpaka asilimia 25 kufikia mwaka 2028.


Mpango huu unakuja kufuatia uwepo wa kiwango cha juu cha udumavu mkoani Kagera kwa asilimia 34.3 huku kukiwa na hali ya ukondefu kwa watoto, watoto kuwa chini ya uzito pale wanapozaliwa na upungufu wa damu kwa watoto chini ya miaka 5.


Mikakati hii itaangazia masuala ya udumavu na lishe kwa watu wote na kuleta matokeo chanya kwa Wanawake,Wanaume na Watoto kufikia mwaka 2028.


Katika kuhakikisha hilo linatendeka Halmashauri zote zimekuja na na mipango mikakati kuongeza wigo wa kutoa elimu ya lishe hadi ngazi za vitongoji na vijiji, kushirikisha jamii katika maeneo yenye changamoto,kuhusisha sekta binafsi, kuongeza uzalishaji wa mbegu zilizorutubishwa kama maharage,mchele,  kusaga unga ulioongezwa virutubisho na kuhamasisha jamii kutumia teknolojia katika uzalishaji kupitia kilimo cha umwagiliaji,bustani ndogo ndogo na ufugaji wa kisasa.


Wadau mbalimbali wanatarajiwa kushiriki katika mpango huu ikiwemo Serikali kupitia TAMISEMI na Wizara ya Afya, kata na Vijiji, Jamii pamoja na sekta binafsi.


Kikao hiki kimehudhuriwa na Kaimu katibu tawala mkoa wa Kagera,Menejimenti ya Mkoa, Wakurugenzi wa Halmashauri, mganga mkuu wa Mkoa, waganga wakuu wa Wilaya,Maafisa elimu sekondari na msingi,maafisa lishe,pamoja na maafisa mipango.



Mkoa wa Kagera kulinga na sensa ya mwaka 2022 ina wakazi wapatao 2,989,299 wanaoishi katika Wilaya za Biharamulo, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba,Manispaa ya Bukoba, Karagwe,Muleba,Ngara,Kyerwa na Misenyi.

Matangazo Madogo Madogo

  • UMITASHUMTA July 20, 2022
  • UJUMBE WA SENSA TOKA KWA MKURUGENZI MTENDAJI BDC July 23, 2022
  • MWENYEKITI NA SENSA July 23, 2022
  • MRADI WA WODI ZA UPASUAJI July 23, 2022
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • BUKOBA DC YAZINDUA VAZI LA IJUMAA

    August 15, 2025
  • BUKOBA DC YAZINDUA VAZI LA IJUMAA

    August 15, 2025
  • KAGERA KUJA NA MPANGO MKAKATI KUPUNGUZA UDUMAVU

    August 15, 2025
  • KAMATI ZA MAAFA BUKOBA DC ZANOLEWA

    July 22, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fomu mbali mbali
  • Picha mbali mbali
  • We are Implementing 2017 (Picha)

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  • Tovuti ya Wizara ya Afya
  • Tovuti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania

Waperuzi Walipo

world map hits counter

Kihesabu Waperuzi

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Bujunangoma

    Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera

    Simu ya Mezani: 028-2220287

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.