• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba District Council
Bukoba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zitolewazo
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Ugani Kilimo
    • Huduma Ugani za Mifugo na Uvuvi
    • Mikopo ya Vikundi vya Wanawake na Vijana
  • Madiwani
    • Madiwani wa Sasa Waliochaguliwa
    • Kamati za Halmashauri
    • Mitasari ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Mfuko wa Taifa wa Maendeleo wa Jamii (TASAF)
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Sheria
    • Ripoti
    • Fomu Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Maktaba ya Picha

KAMATI ZA MAAFA BUKOBA DC ZANOLEWA

Tarehe ya Kuwekwa: July 22nd, 2025

Na Abel Shema

Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Erasto Sima amefungua mafunzo ya kamati elekezi na kamati ya wataalam ya maafa ya Wilaya.

Mafunzo hayo yamefanyika katika ukumbi wa makao makuu ya Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Julai, 21,2025.

Akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh.Sima alieleza kamati elekezi na kamati za wataalam zina jukumu kubwa sana la kuratibu na kushughulikia suala la maafa Wilayani Bukoba.

Sima alieleza maafa wakati mwingine hayapigi hodi, elimu ya leo itakua muhimu sana kwa sababu wakati mwingine majanga yakitokea tumekua tukiulizana tunaanza kuyashughulikia vipi haswa ikizingatiwa Wilaya yetu imekua ikikikumbwa na majanga ya mafuriko,tetemeko,upepo mkali pamoja na radi.

‘’Miezi mitatu iliyopita tulipata mvua ya upepo  watu walipoteza maisha na kuharibikiwa na mazao yao katika kata ya Kishanje, tulikabiliana  na majanga hayo kwa uzoefu lakini sasa tutapata mafunzo  na muongozo sahihi wa kujikinga ,kukabiliana,na kurejesha hali za maisha ya awali kwa waathirika wa majanga ‘’ alisema Sima.

Nae mwezeshaji kutoka ofisi ya Waziri Mkuu Bi. Winniefrida Ngowi alieleza lengo la Serikali ni kuhakikisha kamati za maafa za Wilaya zinajiandaa kikamilifu na kuchukua hatua stahiki za kuzuia majanga yanayoepukika na kuandaa mipango madhubuti ya kukabiliana na majanga ya asili kama tetemeko na mafuriko.

Bi.Ngowi aliongeza kuwa mafunzo haya yatajikita Zaidi katika kutambua majukumu ya kamati ya elekezi ya maafa pamoja na majukumu ya kamati ya wataalam katika kukabiliana na maafa.

Nae mwakilishi wa shirika la World Vision Bi. Jackline Kaihula alisema shirika hilo limejikita katika kuhakikisha jamii na kaya zinaweza kujikimu kwa kipato kwa kuwapatia mikopo ya kuanzisha na kukuza biashara ili hata wanapopata majanga wanaweza kuamka tena.

Mafunzo haya yameratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu kwa Kushirikiana na shirika la World Vision na kuhudhuriwa na kamati ya usalama ya Wilaya pamoja na menejimenti ya Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.


Matangazo Madogo Madogo

  • UMITASHUMTA July 20, 2022
  • UJUMBE WA SENSA TOKA KWA MKURUGENZI MTENDAJI BDC July 23, 2022
  • MWENYEKITI NA SENSA July 23, 2022
  • MRADI WA WODI ZA UPASUAJI July 23, 2022
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI ZA MAAFA BUKOBA DC ZANOLEWA

    July 22, 2025
  • TAARIFA YA UTEKELEZAJI WA SHUGHULI ZA HALMASHAURI KWA KIPINDI CHA MWAKA 2020-2025

    July 11, 2025
  • BUKOBA DC YAZINDUA CHANJO YA KUKU

    July 01, 2025
  • MAPATO JUU,HATI SAFI MEZANI

    June 16, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fomu mbali mbali
  • Picha mbali mbali
  • We are Implementing 2017 (Picha)

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  • Tovuti ya Wizara ya Afya
  • Tovuti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania

Waperuzi Walipo

world map hits counter

Kihesabu Waperuzi

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Bujunangoma

    Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera

    Simu ya Mezani: 028-2220287

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.