• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba District Council
Bukoba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zitolewazo
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Ugani Kilimo
    • Huduma Ugani za Mifugo na Uvuvi
    • Mikopo ya Vikundi vya Wanawake na Vijana
  • Madiwani
    • Madiwani wa Sasa Waliochaguliwa
    • Kamati za Halmashauri
    • Mitasari ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Mfuko wa Taifa wa Maendeleo wa Jamii (TASAF)
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Sheria
    • Ripoti
    • Fomu Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Maktaba ya Picha

Kikao cha Kamati ya Lishe cha Halmashauri ya Wilaya Bukoba

Tarehe ya Kuwekwa: May 20th, 2021

WAJAWAZITO KUNYWENI KWA USAHIHI DAWA MPEWAZO KLINIKI

Afisa Lishe wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera Bibi Victoria Ngatunga amewasihi wadau wa Afya na Lishe wa Halmashauri ya Wilaya Bukoba kusisitiza matumizi ya dawa za Asidi ya Foliki na Madini ya Chuma zitolewazo kliniki kwa wajawazito ili kusaidia uumbikaji  mkamilifu wa viungo vya mwili wa mtoto awapo tumboni.

Bibi Victoria ameyasema hayo leo katika Kikao cha Kamati ya Lishe cha Halmashauri ya Wilaya Bukoba kilichofanyika katika Ukumbi wa Kamati wa Halmashauri ya Wilaya Bukoba ambapo pia amesisitiza wajawazito kuanza mapema kuhudhuria kliniki mara tu baada ya kugundua kwamba ni wajawazito ili waweze kupata huduma stahiki kwa ajili yao na watoto waliomo tumboni.

Katika kuelezea madhara yanayoweza kusababishwa na wajawazito kutotumia dawa za Asidi ya Foliki na Madini ya Chuma, Bibi Victoria alieleza mifano ya vichanga watatu ambao mwanzoni mwa mwaka huu walifikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Kagera wakiwa na mapungufu katika viungo vyao vya mwili ambapo kichanga mmoja alizaliwa bila macho kabisa, mwingine alikuwa na tumbo wazi na mwingine alikuwa na mgongo wazi.

Mifano hii hai iliwagusa sana wadau wa Afya na Lishe waliokuwa wamehudhuria kikao hicho  na wakaazimu kuendelea kuwahamasisha wajawazito kutumia dawa za Asidi ya Foliki na Madini ya Chuma kwa usahihi huku wakiwaonesha shuhuda za vizazi vilivyoathirika kwa kutotumia dawa hizo kikamilifu na kuwasihi wanaume wawahimize wake zao kuhudhuria kliniki na kuhakikisha wanakunywa dawa wanazopewa huko kliniki.

Naye Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya Bukoba ndugu Desidery Karugaba akasema tafiti za hivi karibuni zinaonesha kwamba asilimia arobaini na nne tu (44%) ya wajawazito nchini ndio hutumia kikamilifu dawa za Asidi ya Foliki na Madini ya Chuma huku wasiotumia wakilalamikia ladha mbaya ya dawa hizo na kichefuchefu kuwa chanzo kikubwa cha wao kutozitumia. Hivyo basi ili kuepuka hilo wajawazito wameshauriwa kunywa dawa hizo wakati wa usiku kabla ya kulala badala ya asubuhi.

Mapendekezo mengine yaliyotewa na Kamati hiyo ya Lishe ni pamoja na shule za Msingi na Sekondari kuendelea kutengeneza bustani za jikoni ili kusaidia wanafunzi waweze kujifunza kwa vitendo jinsi ya kulima bustani za mbogamboga, Idara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na Idara ya Maendeleo ya Jamii kuhimiza wananchi kutumia kwa chakula mazao wanayoyazalisha badala ya kuzalisha kwa ajili ya kuuza na kupata faida huku afya za familia zao zikizorota.

MWISHO

Pichani ni baadhi ya Wakuu wa Idara mbalimbali za Halmashauri ya Wilaya Bukoba wakiwa katika Kikao cha Lishe cha Halmashauri hiyo. 

Hawa ni baadhi ya wadau wa afya lishe waliohudhuria katika kikao cha Kamati ya Lishe cha Halmashauri ya Wilaya Bukoba leo


Matangazo Madogo Madogo

  • UMITASHUMTA July 20, 2022
  • UJUMBE WA SENSA TOKA KWA MKURUGENZI MTENDAJI BDC July 23, 2022
  • MWENYEKITI NA SENSA July 23, 2022
  • MRADI WA WODI ZA UPASUAJI July 23, 2022
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • KILA KHERI LA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA MAPENDEKEZO YA MATUMIZI YA FEDHA ZA MAUZO YA ENEO LA CHEMBA.

    April 17, 2025
  • DR.NDUMBARO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO BUKOBA DC

    April 16, 2025
  • KAMATI YA FEDHA NA MIPANGO YAKAGUA MIRADI YENYE THAMANI YA BILIONI 1.1

    April 10, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fomu mbali mbali
  • Picha mbali mbali
  • We are Implementing 2017 (Picha)

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  • Tovuti ya Wizara ya Afya
  • Tovuti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania

Waperuzi Walipo

world map hits counter

Kihesabu Waperuzi

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Eneo la Kemondo (Mubembe S/M)

    Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera

    Simu ya Mezani: 028-2220287

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.