Na Abel Shema.
Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba imeazimisha siku ya mazingira Duniani kwa kupanda miti mia tano katika Hospitali ya Wilaya.
Akifungua zoezi hilo kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmshauri ya wilaya ya Bukoba Dkt Kisanga Makigo alihimiza taasisi na watu binafsi kuendelea kupanda miti ili kuhifadhi mazingira na kupambana na mabadiliko ya hali ya hewa.
‘’Tumechagua kupanda miti eneo la Hospitali kwani kuna uhitaji mkubwa wa miti ya matunda na vivuli ambayo itasaidia kutunza mazingira na kuboresha afya’’.
Nae afisa mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ndugu Dominic Ruta, alieleza miti Zaidi ya mia tano imepandwa ikijumuisha maparachichi,machenza na miti ya vivuli, huku akisistiza zoezi hili ni endelevu.
Kadhalika muuguzi mkuu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ndugu Elizeus Ezra aliishukuru halmashauri na wadau kwa kujitoa kuja kupanda miti hospitalini hapo ambapo itasiaidia kuboresha afya za watumishi na wagonjwa.
Maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani hufanyika juni,05 kila mwaka, na kwa mwaka huu yanaongozwa na kauli mbiu isemayo
‘’Mazingira yetu na Tanzania ijayo,Tuwajibike sasa, Dhibiti matumizi ya plastiki’’
Bujunangoma
Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera
Simu ya Mezani: 028-2220287
Simu ya Mkononi:
Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz
Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.