• Wasiliana Nasi |
    • MMM |
    • Barua Pepe |
    • Malalamiko |
Bukoba District Council
Bukoba District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
    • Maadili ya Msingi
  • Utawala
    • Muundo wa Kiutawala
    • Idara
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Maeneo ya Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
  • Huduma Zitolewazo
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Leseni
    • Huduma za Ugani Kilimo
    • Huduma Ugani za Mifugo na Uvuvi
    • Mikopo ya Vikundi vya Wanawake na Vijana
  • Madiwani
    • Madiwani wa Sasa Waliochaguliwa
    • Kamati za Halmashauri
    • Mitasari ya Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Inayoendelea
    • Mfuko wa Taifa wa Maendeleo wa Jamii (TASAF)
    • Mfuko wa Jimbo
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Kanuni
    • Sheria
    • Ripoti
    • Fomu Mbali Mbali
  • Kituo cha Habari
    • Habari kwa Umma
    • Maktaba ya Picha

WALENGWA TASAF WATEKELEZA MIRADI YA AJIRA ZA MUDA MFUPI

Tarehe ya Kuwekwa: May 29th, 2025

Na Abel Shema.

Walengwa wa mpango wa kunusuru kaya maskini (TASAF) katika Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba wameibua na kutekeleza miradi jamii katika kata zote 29.

Katika mpango huu jamii huibua miradi na kutekelezwa na kaya maskini zinazotambuliwa katika kijiji husika kisha kulipwa ujira baada ya utekelezaji ambao kila kaya hushiriki kwa siku 10 tu kwa mwezi na kulipwa kiasi cha shilingi 30,000

Miradi hiyo inahusisha  ukarabati wa barabara,upandaji miti,uboreshaji wa vyanzo vya maji,uchimbaji wa visima na mabwawa.

Lengo la programu hii ya kuibua miradi ya ajira za muda mfupi ni kupunguza umaskini,kuwapa ujuzi,kutoa ajira kwa walengwa,kuwafundisha namna ya kujitegemea na kuwezesha walengwa kukidhi mahitaji yao.

Walengwa huchaguliwa kupitia mkutano wa kijiji ambao wawezeshaji wanatoa elimu juu ya miradi itakayofanyika na walengwa watakaohusika pamoja na kutoa fursa kwa kijiji kuibua aina ya mradi ambao utatekelezwa na walengwa wa TASAF kijijini hapo.

Vigezo vya kufanya kazi katika mpango huu wa ajira za muda ni pamoja na kuwa na umri kati ya miaka 18 hadi 65, asiwe mtu mwenye ulemavu, asiwe mwenye ugonjwa wa kudumu ama wa muda mrefu .

Mafanikio ya jumla ya mpango huu ni upatikanaji wa miundo mbinu bora ya brabara za vijijini zilizoibuliwa na kuboreshwa na walengwa wa TASAF,kaya za walengwa walioshiriki wanapata ruzuku hivyo kumudu mahitaji yao, kuboresha lishe kupitia programu za upandaji miti ya matunda,walengwa wamepata ujuzi kupitia upandaji miti,uboreshaji wa barababara,uchimbaji visima,kupitia shughuli hizi wamekua na mchango mkubwa kwa jamii katika eneo la miundombinu ya barabara,maji na uhifadhi wa mazingira hivyo imeondoa dhana ya jamii kuwaona ni watu wanaopewa tu fedha bila kujishughulisha.


Matangazo Madogo Madogo

  • UMITASHUMTA July 20, 2022
  • UJUMBE WA SENSA TOKA KWA MKURUGENZI MTENDAJI BDC July 23, 2022
  • MWENYEKITI NA SENSA July 23, 2022
  • MRADI WA WODI ZA UPASUAJI July 23, 2022
  • Tazama Zaidi

Habari Mpya

  • WALENGWA TASAF WATEKELEZA MIRADI YA AJIRA ZA MUDA MFUPI

    May 29, 2025
  • KIKAO CHA TATHMINI YA MKATABA WA AFUA ZA LISHE NGAZI YA JAMII ROBO YA TATU 2024/2025

    May 09, 2025
  • KILA KHERI LA KIDATO CHA SITA

    May 04, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI LARIDHIA MAPENDEKEZO YA MATUMIZI YA FEDHA ZA MAUZO YA ENEO LA CHEMBA.

    April 17, 2025
  • Tazama Zaidi

Video

Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Fomu mbali mbali
  • Picha mbali mbali
  • We are Implementing 2017 (Picha)

Tovuti Mashuhuri

  • Tovuti ya Wizara ya Utumishi na Utawala Bora
  • Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
  • Tovuti ya Wizara ya Afya
  • Tovuti ya Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani Tanzania
  • Tovuti ya Baraza la Elimu ya Ufundi Tanzania

Waperuzi Walipo

world map hits counter

Kihesabu Waperuzi

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Bujunangoma

    Anuani ya Posta: P.O.Box 491 Bukoba - Kagera

    Simu ya Mezani: 028-2220287

    Simu ya Mkononi:

    Barua Pepe: ded@bukobadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Disclamer
    • MMM
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Hati Miliki 2018 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba.Haki zote zimehifadhiwa.